July 24, 2021

 


HABARI ikufikie kuwa uongozi wa Yanga

umeamua kubadili rasmi mipango ya kutua

nchini kwa wachezaji Shabani Djuma na Fiston Mayele ambao walitakiwa kutua mapema wiki

hii.


Yanga tayari ilikwishamalizana na Shabani

Djuma ambaye alikuwa ni beki wa kulia wa AS

Vita mara baada ya kumsajili kwa mkataba wa

miaka miwili huku Fiston Mayele yeye akikiri

wazi kuja kukamilisha dili na Yanga pindi

atakapotua nchini sambamba na Shabani

Djuma.


Chanzo chetu cha uhakika kutoka Yanga

kimeliambia Championi Ijumaa kuwa sababu

kubwa ya kubadili siku ya wachezaji hao kutua

nchini ni uwepo wa fainali ya Kombe la

Shirikisho la Azam Sports (ASFC) dhidi ya Simba

ambapo inaweza kuleta presha kwa wachezaji

ambao wapo kwa sasa, hivyo ujio wao utakuwa

mara baada ya kumalizika kwa fainali hiyo.


“Ilikuwa ni mipango yetu kuona wachezaji hao

wanakuja na kushuhudia mchezo wa fainali

dhidi ya Simba lakini tumeona itawaongezea

presha kubwa wachezaji ambao wapo kwani

kama ambavyo unafahamu kwa sasa ni mwisho

wa msimu, kuna mambo ya kuachana na

wachezaji na kuingiza wachezaji wapya.


“Hivyo baada ya kumalizika kwa mchezo huu,

tunatarajia wachezaji hao kuingia hapa nchini

kwa ajili ya taratibu mbalimbali za timu

ikiwemo mipango ya maandalizi ya msimu

ujao,” kilisema chanzo hicho.


Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa

Yanga, Dominick Albinus, alisema kuwa uongozi

wa klabu hiyo hautarajii kumpokea mchezaji

mpya yeyote ndani ya klabu hiyo kwa sasa

labda mpaka kumalizika kwa mchezo wa fainali

dhidi ya Simba mara baada ya ligi kumalizika.


“Ligi tayari ilishamalizika, kilichobaki kwa sasa

ni kumalizika kwa mchezo wa Kombe la

Shirikisho tutakaocheza dhidi ya Simba huko

Kigoma, ndio mambo mengine yaweze

kufanyika kwa kufuata taratibu maalumu

zilizoandaliwa na uongozi wa Yanga.


“Kuhusu wachezaji wapya kuja kuutazama

mchezo wa fainali dhidi ya Simba niseme

hapana hakuna mpango kama huo kwa timu

labda mpaka fainali hii itakapomalizika ndio

tunatarajia kuona wachezaji wapya wakianza

kutua nchini,” alisema kiongozi huyo.

2 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic