July 24, 2021

 


UNAKUMBUKA ile posho ya milioni 500 ambayo

uongozi wa Yanga uliwaahidi wachezaji na

benchi la ufundi endapo wataifunga Simba

katika mchezo wa Ligi Kuu na Yanga

wakafanikiwa kuifunga?


 Sasa unaambiwa matajiri wa Yanga wameweka kiasi hicho hicho ili waifunge tena Simba katika mchezo wafainali ya FA itayochezwa kesho Julai 25, mkoani Kigoma.

Hivyo ramani ya Simba kufungwa imechorwa na mabosi kupitia mkwanja mrefu uliowekwa mezani ikiwa wataweza kuwafunga watani zao hao wa jadi.


Yanga katika mchezo uliopita dhidi ya Simba

walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0

katika mchezo wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu

Bara kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar, huku

mchezo wa safari hii katika fainali ya Kombe la

Shirikisho la Azam Sports ukitarajiwa kufanyika

katika Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani

Kigoma.


Chanzo chetu cha ndani ya Yanga kimeliambia

Championi Ijumaa kuwa uongozi wa Yanga

umeweka ahadi kama waliyoiweka katika

mchezo ule wa kwanza ambao Yanga ilifanikiwa

kuibuka na ushindi wa bao 1-0 huku wakiamini

pia kiasi hicho kitatosha kuwapa motisha

wachezaji na kupata ari ya kupambana na

kuibuka na ushindi dhidi ya wapinzani wao.


“Uongozi wa Yanga umetoa ahadi kama ile ya

mwanzo ambayo ilisababisha Yanga iweze

kuibuka na ushindi dhidi ya Simba, kama

unakumbuka kiasi cha awali katika mchezo

uliopita ilikuwa ni milioni 500 jambo ambalo na

safari hii uongozi umeamua kuweka kiasi

hichohicho.


“Sababu kubwa ya kufanya hivyo kwa viongozi

wanaamini kuwa kiasi hicho kinatosha kuwapa

wachezaji ari ya kupambana na kuipatia ushindi

timu kama ambavyo ilivyotokea mara ya

kwanza ambapo Yanga ilifanikiwa kuibuka na

ushindi katika mchezo wa ligi,” kilisema chanzo

hicho.


Alipotafutwa Dominick Albinus ambaye ni

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga

alisema kuwa ahadi na posho za wachezaji na benchi la ufundi la Yanga kuelekea katika mchezo wa Yanga zinabaki kuwa siri kutokana na mambo mbalimbali ambayo yamekuwa yakijitokeza baada ya ahadi hizo.


“Kuhusu ahadi kuelekea mchezo wetu wa fainali dhidi ya Simba inabaki kuwa ni siri kati ya viongozi wa timu, benchi la ufundi na wachezaji kwani mara nyingi mara baada ya kutangaza ahadi mambo mbalimbali hujitokeza ambayo tumekuwa tukiyalaani sisi kama viongozi,” alisema kiongozi huyo.

6 COMMENTS:

  1. Hoyo ndio ramani, nilidhani no tactics za uchezaji kumbe motisha. Sawa.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hiyo ndio mchoro. Na kiasi kidoogo alikula refa kuhakikisha anatibua kila move itayoweza kuleta madhara. Yupo mchezaji mmoja alikuwa anajua wapi refa anapatikana....... ila AA kidogo kuna mashaka simu yake haipatikani

      Delete
  2. Wasikilizeni waandishi kama kawaida ya watu wenye mihemko ya mikia kupinda

    ReplyDelete
  3. Wazee wa kuishia kuchora ramani ile ramani ya ubingwa iliishia wapi

    ReplyDelete
  4. dirayamafanikio.blogspot.com

    ReplyDelete
  5. Mchora ramani hakueepo kwenye ligi kuu?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic