August 3, 2021


BREAKING: DILI la usajili wa mshambuliaji wa zamani wa Horoya AC ya Guinea, Heritier Makambo limekamilika ambapo leo ametabulishwa rasmi ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi.

 

Makambo ni kati ya wachezaji waliokuwa kwenye mipango ya kusajiliwa na Yanga katika usajili wa msimu huu katika kuisuka safu ya ushambuliaji ya timu hiyo.

 

Nyota huyo anaijua sera ya Yanga kwa kuwa  alisepa hapo msimu wa 2018/2019.


Mshambuliaji huyo amepewa dili la miaka miwili ndani ya Yanga.


Makambo alitua Bongo Juzi kwa ajili ya kumalizana na mabosi wa Yanga na baada ya kukamilisha utaratibu wa mwisho amesaini ndani ya timu hiyo ambayo inajiimarisha kwa ajili ya msimu ujao na itashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.

 


4 COMMENTS:

  1. Ndio hili jambo la leo la wananchi? Tomu inaongozwa kiswahili swahili tuu

    ReplyDelete
  2. Yanga kumsajili makambo ni sawa na simba kumsajili okwi, hawana jipya hao.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Okwi atacheza FDL lkn Makambo atacheza Premier League hiyo ndio tofauti tarehe 24 haiko mbali CAS hoyeee

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic