August 1, 2021


 IMERIPOTIWA kwamba bei ya nyota wa Chelsea Tammy Abraham imeshushwa ili aweze kuuzwa kwa timu ambayo inamuhitaji ambapo Arsenal inapewa nafasi kubwa ya kumpata mshambuiaji huyo kwa dau ambalo linaweza kuwa chini ya pauni milioni 40.

Awali mabosi wa Chelsea walikuwa wanahitaji kupewa pauni milioni 40 kwa ajili ya kumuuza mchezaji huyo ila mambo yamekuwa tofauti sokoni kwa kuwa anaonekana kudoda.

Abraham mwenye miaka 23 hajawa na nafasi kikosi cha kwanza baada ya timu hiyo ya Chelsea kuchukuliwa na Kocha Mkuu, Thomas Tuchel ambaye alishinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Ni pauni milioni tano ambazo inaripotiwa kwamba Chelsea inayotumia Uwanja wa Stamford Bridge kwenye mechi zake za nyumbani inapanga kuzikata jumla ili aweze kuibukia ndani ya Uwanja wa Emirates msimu ujao.

Mikel Arteta Kocha Mkuu wa Arsenal inaelezwa kuwa amekuwa njia panda ili aweze kumsajili mchezaji huyo kwa kuwa wanaona kwamba gharama iliyopunguzwa ni kubwa mpaka kufikisha dau la pauni milioni 35.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic