September 28, 2021

 


SEPTEMBA 28, Ligi Kuu Bara inaendelea kuchanja mbuga baada ya jana Septemba 27 kuanza kasi kwa timu tatu kupambana kusaka pointi tatu. 


Simba inayonolewa na Kocha Mkuu,  Didier Gomes itakuwa Uwanja wa Karume, Mara bila uwepo wa nyota wao Taddeo Lwanga ambaye alionyeshwa kadi nyekundu katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga, Uwanja wa Mkapa, Septemba 25.


Mbali na mchezo huo unaosubiriwa kwa shauku kubwa pia Dodoma Jiji itakuwa na kibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya Ruvu Shooting,  Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. 


Pia kuna mchezo mwingine ambapo Mbeya City itakuwa na kibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya Tanzania Prisons,  Uwanja wa Sokoine.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic