ALIYEWAHI kuwa Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, ambaye kwa sasa ni msemaji wa Yanga, amemtaka kiungo wa Simba, Bernard Morrison amjibu kuhusu suala la Mohamed Dewji kujiuzulu nafasi ya uenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi.
Manara amemtaka Morrison amjibu baada ya mchezaji huyo kuwa na tabia ya kujibu kwenye mtandao wa Instagram wa Manara.
Manara ameibua hoja hiyo baada ya bilionea Mo Dewji kujiuzulu kwenye nafasi yake ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba na kubaki kama muwekezaji.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Manara amemuuliza hivi Bernard Morrison; “Bernard nimemisi kuona ukinijibu kwenye akaunti yangu, hebu niambie kipi kimemfanya Muhamedi kujiuzulu au ni zile bilioni mbili wanazomuuliza aliziweka kwenye akaunti gani ya benki ndio maana kajiuzulu maana hapendi kuulizwa.”
Morrison naye akamjibu hivi Manara;“Kuna msitari kwenye Biblia unasema kuwa nabii huwa haheshimiki kwao, kwa hiyo sijashtuka kuona unahangaika kuzidi kuipaka matope heshima ya Mohamedi
“Tafuta kampuni yoyote ya kwako au hata mwambie Injinia Hersi Said akusaidie angalau uwe na kampuni maeneo ya Mikocheni ili walau ukae kwenye levo za Mohamedi, natamani kucheka ila imoji hazitembei.”
Manara aneshajishushia hata ile heshima kidogo aliyokuwa nayo, watu wanamhurumia tuu
ReplyDeleteKatika wajinga Manara ni kinara wao.Jambo halimhusu amevalia njuga.Simba wameshakutema bakia huko huko.
ReplyDeleteNa jamaa wanaona wamempata wa kuipa mafanikiotimu
ReplyDeleteMjinga ni yule anaejifanya anajua kumbe kiazi. Manara anaupiga mwingi mpaka kawachanganya MO sports
ReplyDeleteAliye kaa kimyaa ndio mwerevu,wengine wote wajinga akiwemo MANARA na wewe unaebishana hapa.na ukitaka kuona ujinga wako lazoma utatoa povu kama sabun ya unga.
ReplyDeleteManara yupo sahihi..Mtu kama Morrison hakutakiwa kujiingiza kwenye migogoro ya kimtandao, yeye ni professional prayer aangalie mstakabali wa mpira tu..kujibizana na watu nje ya dimba naona hakumstahili km mchezaji wa kimataifa!acheze mpira.
ReplyDeleteUyo manala yupo saikwako Leo sio sisi simba
ReplyDeleteUyo manala yupo saikwako Leo sio sisi simba na kama kweli piya yupo said mfungulie ofisi basi
ReplyDeleteHeheheee manara anaupiga mwingi
ReplyDeleteMorrison ana akilu Sana majibu yake Yana mafundisho Sana. Inabidi Manara ajifunze kitu hapo aachane na Mo huyo sio saizi yake Ni mtu aliyemuinua ktika ulimwengu wa soka.
ReplyDeleteHivi kesi ya Morrison Na YANGA niaje jamani ???
Delete