October 27, 2014


Amri Kiemba, Shabani Kisiga na Haruna Chanongo wameamriwa kuondoka kwenye kambi ya na kurejea jijini Dar es Salaam.

Wachezaji hao watatu wanatuhumiwa kwa utovu na taarifa zinaeleza kuwa asubuhi wataondoka kurejea Dar es Salaam kwa mabasi.

Uamuzi huo umefikiwa kwa pamoja na wajumbe wa kamati ya utendaji ya Simba wanaowatuhumu kwa utovu wa nidhamu.
Baada ya hapo, wametakiwa kurejea Dar es Salaam na Ijumaa ikiwa ni siku moja kabla ya Simba kuivaa Mtibwa Sugar mjini Mororogo, wenye watawekwa kiti moto.
Wachezaji hao watawekwa kitimoto na kamati ya utendaji ya Simba kuhojiwa kuhusiana na masuala ambayo yameelezwa ni ya utovu wa nidhamu.
Viongozi wa Simba wamekuwa wagumu kulieleza hilo, lakini taarifa zinasema iwapo kutabainika kuna tatizo, basi wachezaji hao wataondolewa kabisa katika kikosi cha Simba.
Simba imetoka sare tano katika mechi zake tano, nne ikiwa imecheza nyumbani hali inayosababisha presha kubwa Msimbazi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic