Kikosi cha Simba kinaondoka mjini Mbeya na
kwenda kuweka kambi mjini Iringa.
Kikosi cha Simba kinatokea mkoani Mbeya ambako kilicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu Bara nje ya Dar na kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Prisons.
Simba inakwenda kuweka kambi kwa siku mbili mkoani
Iringa kabla ya kuondoka kwenda Morogoro tayari kuivaa Mtibwa Sugar.
Mtibwa Sugar pia iko Mbeya ambako ilicheza
mechi dhidi ya Mbeya City na kuitungua kwa mabao 2-0.
Mtibwa imekuwa inakwenda na mwendo mzuri
huku ikishinda mechi zake kwa asilimia 90.
Hali inayowalazimu Simba waliotoka sare tano
katika mechi tano kutakiwa kujiandaa vilivyo.
“Kweli tutaanza safari ya kwenda Iringa
ambako tutaweka kambi,” kilieleza chanzo.
0 COMMENTS:
Post a Comment