June 11, 2016


MNYATE
Kuna taarifa za uhakika kwamba Simba imefanikisha usajili wa mshambuliaji wa Mwadui FC, Jamal Mnyate kwa dau la Sh milioni 15 tu.

Mnyate ndiye aliyeitoa Simba kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara kutokana na bao lake alilowafunga kwenye mechi ya raundi ya pili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mwadui ilishinda bao 1-0. 

Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya Simba zinaeleza mshambuliaji huyo amesaini mkataba wa miaka miwili kwa dau hilo la usajili akiwa kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba Mwadui. 

“Mnyate tumemalizana naye kama wiki moja iliyopita, amesaini mkataba wa miaka miwili ya kuichezea Simba kwa dau la Sh milioni 15.

“Tulimsajili kama mchezaji huru kutoka Mwadui FC mara baada ya mkataba wake kumalizika wa kuichezea timu hiyo,” kilisema chanzo hicho.

Alipotafutwa mshambuliaji huyo kuzungumzia usajili wake, alikiri kusaini Simba huku akigoma kukubali au kukataa kuhusu dau la usajili. 


“Siwezi kutaja kiasi nilichosainia Simba kwani fedha ya usajili ni siri kati yangu na klabu, hivyo siwezi kuzungumzia hilo,” alisema Mnyate.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic