July 7, 2016


Cristiano Ronaldo amefunga bao moja na kutengeneza moja na kuiwezesha Ureno kutinga fainali ya Euro kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Wales.

Ronaldo ndiye alifunga bao la kwanza katika dakika ya 50 na kusababisha la pili lililofungwa na Louis Nani na kuzima ndoto za Wales iliyokuwa ikiongozwa na Gareth Bale anayekipiga timu moja ya Real Madrid na Ronaldo.

Awali, kulikuwa na ubishi, nani kati ya Ronaldo na Bale atatinga fainali. Ingawa Bale alionyesha kiwango bora kabisa lakini sasa jibu liko hadharani.

Hadi inatinga nusu fainali, haikuwa imeshinda hata mechi moja ndani ya dakika 90. Pia ilivuka hatua ya makundi ikiwa best looser.

Leo imeshinda kwa mara ya kwanza ndani ya dakika 90 na kufanikiwa kutonga fainali.





















0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic