UONGOZI wa Simba umebainisha kuwa utarejea ukiwa imara kwa ajili ya kuendelea na mapambano ndani ya uwanja kwa msimu wa 2021/22.
Jana, Septemba 25, Uwanja wa Mkapa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza kesho Septemba 27 walipoteza kwa kufungwa baoa 1-0 dhid ya Yanga.
Ilikuwa ni kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii ambao ulikuwa ukisubiriwa kwa shauku kubwa na mashabiki wa Tanzania na nje ya Tanzania.
Jitihada za Simba kupindua meza kuweka usawa mzani kwa bao lililofungwa na Fiston Mayele dakika ya 10 ziligonga mwamba kwa kuwa mbinu za Kocha Mkuu, Didier Gomes ziligoma.
Ni Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez amebainisha kwamba watarejea wakiwa imara.
Barbara ameandika namna hii:"Every loss is a teachable moment.(kupoteza ni sehemu ya kujifunza) Tutarudi kwenye ubora wetu Insha’Allah!








Kocha Gomezi tunaomba awe mbunifu wa kuamini na kuwapa nafasi wachezaji wengine wengi mahiri ndani ya kikosi chake kuliko kung'ang'ania wachezaji hao kwa hao kila mechi. Mfano mzuri tumeona kwa Kennedy Juma jinsi alivyoonesha kiwango bora binafsi naona ni wakati muafaka kwa Kennedy Juma kuingia kikosi cha kwanza. Mechi kama ya leo badala ya John Boko kwangu mimi naona Yusufu Muhilu kijana ananguvu anajua kufunga kulikuwa hakuna sababu ya kumueka nje. Simba ina mabeki wengi wa kati kwanini kocha anashindwa kutumia beki watatu kwenye mechi ambyo ni kazi zaidi. Kuna kipindi kocha aliepita wa Simba Vandebrook alipanga, Onyango, Wawa na Ame na alimaliza kabisa tatizo la beki alipohitaji kufanya hivyo.Huyu beki mpya wa kongo Enock hakuna haja ya kumueka nje. Dukani nyoni kwanini asianzishwe mechi?Tatizo nini? Nataka kuona nafasi ya Bwalya akicheza Abdu swamadi na amini yupo sharp na uwezo wa kufanya vyema Zaidi. Tunamuamini Gomezi ila kocha lazima awe mbunifu wa mbinu tofauti.Goli tulilofungwa na Yanga ni aina ya magoli wanaorejea kutufunga kila tunakutana kwa kutumia udhaifu wa kasi ndogo ya mabeki wetu hasa wa kati kwa kushtukiza dakika za mwanzoni mwa mchezo. Hata kule kigoma kama Tusila angekuwa makini kidogo basi yanga wangefunga tena simba goli kama la leo.
ReplyDeleteAsante, tumekusikia. Pole! Tutakupanga wewe mchezo ujao. Utaupiga mwingi mpaka umwagike.
DeleteMtu akitoa mawazo yake amini yeye anaona hivyo ni sawa mwache wakichukua hayo maoni sawa
Deletehuyu anonymous ni mpumbavu fulani HIV mpuuzeni
DeleteMdau upo sahihi kabisa nakuunga mkono kwa asilimia Mia moja,kocha Gomes na wasaidizi wake wanekariri wachezaji,ukiangalia Wawa pumzi Hana kabisa,Shomary Kapombe amekuwa akifanya makosa tangu mechi ya To Mazembe lakini makocha wetu Bado wanamga'aninia ni wakati wa Israel Mwenda kupata nafasi.Beki Mkongo aanze first eleven.Dilunga Jana hakutakiwa kuanza angeanza Peter Banda na tuliona alivyoingia alivyo drible mipira mbele.Nina wasiwasi kocha akiendelea hivi na kukariri wachezaji hata CAF club champion league makundi tunaweza tusiingie
ReplyDeleteMugalu nafasi kibao anakosa hapo utamlaumu kocha?
ReplyDeleteKwa nini asilaumiwe wakati wapo mastriker wengine? Huyuhuyu si ndoo alikoseha nusu finalize wakati anakosa magoli mengi ya wazi? Mugalu ilitakiwa na yeye asianze kikosi Cha Kwanza anaikosesha Simba magoli mengi mno, huwezi kosa magoli karibu Saba kwa mechi moja kwa timu iliyo na strikers zaidi ya wawili afu uzidi kung'ang'ania tu. No kosa la kocha
DeleteMmi nakaa penben sishabikii tena simba mpkawa watambue mugalu anatuangusha saanaa. Wanamgangania wa nin au ni mradi wa mtu
ReplyDeleteMugalu anatakiwa akae benchi kwanza awapishe vijana akina Kibu Denis na Muhilu waoneshe uwezo wao
DeleteKitu kingine shida ya Simba wanapoanza mchezo kipindi cha kwanza huwa wanaridhika sana, hawako makini kutafuta magoli ya mwanzo kama Yanga wanavyokuwa wanaingia kipindi cha kwanza.
DeleteUtaona kabisa mechi mbili za walizoshinda Yanga ni umakini na juhudi kwa kipindi cha kwanza. Siyo Simba mara nyingi wamekuwa wakitumia nguvu na juhudi kipindi cha pili.
Halafu hakukuwa na haja ya Mugalu kucheza kipindi chote kwa sababu alikosa magoli mengi sana lakini pia kwenye kiungo Simba bado pamoja na mabeki.
sahihi sana. km wanakuwa waoga hv cjui shida ni nn yani inauma sana
DeleteThey're not aggressive compare to yanga
DeleteMi naona hiyo ni Hali ya mchezo tu wachezaji na makocha wapewe nafasi mechi za Simba na yanga zina mambo yake zina tamaduni zake ngoja ligi ianze ndio tutakua na nafasi ya kuzungumzia timu yetu sio kwenye hii dabi.
ReplyDeleteWewe uliyeandika UJUMBE HUO HAPO JUU UKO MAKINI NA NIMFUATILIAJI SANA.UKO SAHIHI ASILIMIA ELFU KUMI MAANA UCHUMI WA ZIMBABWE ULISHAWAHI KUPOROMOKA KWA ASILIMIA ELFU SITA.
DeleteSIMBA tusilaumu wachezaji wala koch a
Huwa hizi timu zinapokutana kuna TAMADUNI ZAO ZISIZOELEZEKA.
BY KOMANDOO WA YESU
Hata wewe Komandoo wa Yesu unaamini kwenye hizo tamaduni zisizoelezeka?
Deletewewe sio komando wa yesu kutokana na kuamini tamaduni zisizoeleweka
DeleteYote yaliotangulia ni kweli kabisa shida yangu ni bwalya yaaani sikuelewa kazi ake back pass zilikua nyingi kuliko pasi zenye macho kwenda mbele..bwalya anahitaji kuteam up vizur na sakho wata tengeneza great combination,Simba iache uzembe,coz hata malipo Yao ni mazur they need to prove their worth,wafanye mazoezi ucku na mchana ikibidi mo aeke mataa pale uwanjani bunju wapige zoez la kutosha,aliswma kanute he saw future in Simba,so he need to work hard to get there,pia ni wakati wa kuuza kagere na mugalu ikiwezekana bocco pia,wameipambania Sana Simba but hawawez kutuv XDusha zaidi ya hapa tuliwpo..
ReplyDeleteTunaanza na tempo ya chini sana cku zote hasa game na Hawa jamaa!mwl afanye rotation kwny kikosi chake Kuna watu kwetu Kama kapombe Hussein nk Wana fatique
ReplyDeleteLazima mwaka huu mumfukuze hiyo STD 7B ...nyau...💩💩🤣🤣🤣🤣
ReplyDeleteKama unasumbuliwa na UPUNGUFU wa NGUVU ZA KIUME au KISUKARI au BLOOD PRESSURE(BP) au UTI WA MGONGO, tumia mchanganyiko huu ndani ya mwezi mzima 👇👇👇👇
ReplyDeletehttps://bit.ly/3kcGG32
Kwann simba mkifungwa msiseme tu yanga wametuzidi hadi kutoa kasoro lukuki?
ReplyDeletenaona kikosi chote mnaweka kipya, hivi haonsi ndio wachezaji wenu wa kila siku?
Kila upande mnakosoa??
Sasa mnatakankusema nyie mna ujuz wa mpira zaid ya Gomez??
mkiona kila mara mkifungwa na yanga ni kulalamika basi kikosi chenu ni bora zaidi na hakuna haja ya kuleta porojo hapa
Asante sana kwa maoni yenu mazuri mm ninaomba mugalu na tadeo lwanga watemwe Simba hawafai ingiza mkude na wengine chipukizi pale hatuna kocha!!
ReplyDeleteKocha anashindwa kabisa kuwajenga wachezaj kua na molari kwenye game za derby maranying sana imekua hvyo kwenye game dhid ya yanga wakat yanga kikos chao nikawaida ila wanapambana kwel... Alafu NAIC kocha gomes cjuh kama anashaurika aiwezekan kila cku ukawa unampanga mugaru ndio chaguo LA kwanza kwake wakat kila cku anakosa magoli yakizembe kabisa tena kwenye game muhim kabisa alafu wakina mk14 awapi nafasi kabisa. mbinu zake ndo zile zile amekua mgumu kubalika anacheza mipira mirefu wakat uyo mugaru mwenyewe mbele galasa katka mafoward wa cmba waliopo pale mugaru ni chaguo LA 4 anauwezo wakuwaweka wale wengine nje ata kidogo Alafu ndo kocha anasema eti ndio foward anaemtemea msimu huu ili team ifanye vizuri.simba Aiwez kwenda popote kwa kumtegemea mugaru. Uwez kuniambia et mugaru mzuri kwakua maveki wa team pinzan awapand alafu anakosa magoli yakipumbavu kabisa foward kipaumbele cha kwanza ni kutupia yule mayele kapata nafasi mbil2 na kafunga bao Leo anaoneka foward mzur na sio kuzuia mabeki.. Kiufup uyu kocha ANATUFERISHA KABISA AMNA KITU...
ReplyDeleteKwa mawazo yako unadhani Chris KOPA MUGALU ANAKOSA MAKUSUDI ???
DeleteJE Wewe UNGEFUNGA ???
UMEISHA WAHI KUCHEZA MPIRA ???
TUWE WATULIVU MPIRA NI MCHEZO WENYE MATOKEO YA KIKATILI YATAKA MOYO SANA.
HALAFU YANGA TULUWAFUNGA KIGOMA NA TUKACHUKUA KOMBE SASA HUO NDIO UTANI SIO KILA MARA ANAADHIBIWA YANGA TU BASI TUTAKUWA HATUNA MTANI .
ILI IWE DABI NI LAZIMA IWE HIVYO CHA MSINGI NI KUKUBALUANA NA MATOKEO .BARIKIWA.MWINGINE ASEMA
UNASEMA INAUMA SANA.
JE WALIVYOGUNGWA KIGOMA NA KUKOSA KOMBE WALIUMIZWA KIASI GANI YANGA???
TULIENI TUINGUE KWENYE LIGI.
BY KOMANDOO WA YESU
Mugalu forward bora hapa nchini na hakuna kama yeye, tusidanganyane, hivi bokko alifanyanin cha maana hata kukaa nanmipira hawezi, nimegundua wachezaji wengi wa simba hawawezi kucheza na mugalu labda sacho na kibu denis
DeleteMpira ni mchezo wa furaha sana, hasa pale upande wenu unaposhinda. Kinyume chake ni maudhi sana. Ili uendelee kupata furaha ya mpira, huna budi kuyakubali matokeo matatu yanayotokeo uwanjani ndani dk 90. Tufike mahali tushauri vzr badala ya jazba na matusi. Ulimwengu wa soka, sio wa sisi Simba peke yetu. Yes, tuendelee kushikamana, hii ya juzi ishaisha, tusonge mbele. Hivyo tu.
DeleteIslaer mwenda,Kennedy,inonga,kanout,mkude,ajibu,sakho,banda,kibu Dennis,hamja haja ya kuumiza kichwa
ReplyDeleteKipa manula sina imani nae na huyo mmoja aliebaki atachagua mwenyewe
ReplyDeleteThe best "The 🦁"
ReplyDeleteKocha na mugalu wachunguzwe
ReplyDeleteTimu yetu ya simba inashida katika safu ya ulinzi makosa ni yaleyale, mabeki hawawezi kuwini mipira ya juu kwa hasa wakiwa wapinzani wamemark man to man, kumekuwa na kujisahau kwa mohammed hussein akipanda harudi mapema, hivyo eneo lake linapokuwa na winga amabaye ni aggressive simba tunafungwa kiurahisi lkn pia eneo la ufungaji striker kama mugalu anawini mipira lkn hana utulivu wa kufunga, anakosa magori mengi kias kwamba kama hakutakuwa na muunganiko mzuri wa sehemu ya attacking midfielders timu kupata matokeo itakuwa vigumu nadhani couch ashughulikie suala la ulinzi na attacking
ReplyDeleteKilio chenu kimesikika ����
ReplyDeleteYani bim yangu ya simba munatuangusha washabiki wenu tatizo nini kwani naona hali si mzuri
ReplyDelete