July 6, 2016


Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom imetoa Sh milioni 6 kudhamini safari ya mafunzo ya wahariri 30 wa michezo nchini ambao wanakwenda nchini Kenya.

Wahariri hao kupitia Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (Taswa) ambao wamepata mwaliko kutoka kwa chama cha Kenya (SJAK), watakwenda jijini Nairobi kwa ziara hiyo ya mafunzo.

Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom, Jacqueline Materu amesema: “Tumeona hii ni fursa njema kusaidia ziara hiyo ambayo itakuwa na faida katika maendeleo ya tasnia ya habari pamoja na michezo.”


Kwa upande wa Taswa, Makamu Mwenyekiti, Egbert Mkoko aliwashukuru Vodacom kwa udhamini huo ambao alisema wameonyesha undugu wa damu.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic