March 17, 2013



Beki wa Chelsea, John Terry ametoa kali ya wiki baada ya kuamua kulitelekeza gari lake lenye thamani ya pauni 175,000 (Sh milioni 437) barabarani na kurejea zake nyumbani.
Nahodha huyo wa Chelsea alichukua aumuzi wa kuliacha gari hilo aina ya Bentley kutokana na foleni kubwa iliyomchosha na kuamua kuliacha.

Lakini kwa wanaoishi Dar es Salaam, kama Terry angeishi angalau mwezi mmoja katika jiji hili maarufu kwa foleni, basi inawezekana kila siku angejikuta akitembea kwa miguu kurejea nyumbani huku agari akiliacha barabarani.


Akiwa katika barabara ya A3, magari hayakuwa yakisogea mbele, hali iliyomfanya aombe msaada kwa mtu anayemfahamu ili aifanye kazi ya kulipeleka kwake iwapo foleni itapungua.

Kabla ya Terry maarufu kama JT kuamua kuliacha gari hilo, watu wengine pia walionyesha kuchoshwa na foleni hiyo na kuteremka kwenye magari yao na kuanza kupiga stori.

Terry aliona hana sababu ya kupoteza muda, hivyo akateremka na kuachana na gari hilo lenye thamani kubwa.

Foleni hiyo kubwa ilisababishwa na mtu mmoja aliyeamua kujirusha darajani ili apoteze maisha. Wakati huo waokoaji walikuwa wamefika katika eneo la tukio kwa ajili ya uoakoaji.

Juhudi zao za kuokoa roho ya mtu huyo ilishindikana baada ya kufia katika gari la wagonjwa wakati madaktari wakijaribu kuokoa uhai wake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic