March 17, 2013




Kama ulikuwa unafuatilia soka ya Tanzania, hakika utakuwa haujamsahau mshambuliaji wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi.

Huyu jamaa ni raia wa Uganda, inawezekana kabisa ndiye alikuwa mchezaji hatari zaidi kuliko wengine wote walioshiriki misimu miwili iliyopita ya Ligi Kuu Bara.


Tokea ameondoka Simba na kujiunga na Etoile du Sahel takribani miezi minne iliyopita, tayari kumekuwa na tatizo kubwa ndani ya klabu hiyo hiyo.


Achana na tatizo la uongozi kulumbana, mfano mkutano wa leo asubuhi Jumapili ambao unanuia kuung’oa uongozi, lakini kikosi cha Simba kimeyumba kabisa!

Uchezaji umebadilika na hata mashambulizi ya Simba yamekuwa si yale yaliyokuwa yakifanyika katika mechi za msimu uliopita.


Hapa cha kujiuliza tatizo ni uwezo wa Okwi umeathiri Simba, au kuondoka kwa aliyekuwa Kocha Mkuu, Milovan Cirkovic. Au mgogoro kati ya viongozi?


Maswali yanaweza kukosa majibu au majibu yakawa ya kujikanganya, lakini siku ya mwisho, Okwi alikuwa mhimili mkubwa wa mashambilizi ya Simba.
Sasa hapo ndiyo pa kuweka swali la msingi, Simba itaendelea kuyumba kwa muda gani bila ya kuwa na Okwi?

Tanzania nzima, hakuna mshambuliaji mwenye uwezo au kipaji kama cha Okwi?
Je, nini cha kufanya baada ya hapo ili kikosi cha Simba kikawe sawa. Hapa kuna mambo mengi sana ya kujifunza kwa Simba ukianzia uongozi wa juu, wachezaji na hata mashabiki we klabu hiyo.

KAZI KWENU.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic