Di Canio
ndiyo alikuwa ameanza kazi ikiwa ni pamoja na kuandamwa na masuala ya kisiasa
kwamba ni shabiki wa siasa za kifashisti. Jana aliendelea kukataa kuzungumzia
masuala hayo baada ya mechi.
Mechi nyingine,
QPR ilipoteza matumaini ya kubaki Premiership baada ya kutoka sare ya bao 1-1
dhidi wageni wake Wigan.
Mambo
yanaonekana si mazuri na kocha Harry Redknapp amekiri kwamba muziki ni mnene
kwao.
Ukiachana na
mechi zote, kali zaidi ilikuwa ile ya Tottenham ilipowakaribisha Everton. Matokeo
ya mwisho yalikuwa 2-2.
Lakini
ngoma ilikuwa si mchezo na timu zote zilicheza mchezo wa kasi ya ajabu,
kushambuliana kila upande na mshambuliaji wa Spurs, Emmanuel Adebayor alikuwa
kiwembe.
Liverpool
nao wakiwa nyumbani Anfield, wakakamatwa na West Ham kwa sare ya bila
kufungana. Wenyeji walionekana kupania kuendeleza ushindi lakini mambo yakawa
tofauti kabisa baada ya wageni kukomaa.
Nayo Newcastle
ikaiathibu Fulham kwa bao 1-0, huku ikifanikiwa kupata ushindi mwishoni. Timu hiyo
imekuwa ikipoteza mwelekeo tofauti na msimu uliopita ilionekana ni kiboko cha
vigogo.
0 COMMENTS:
Post a Comment