Ingawa amewaachia pengo la vituko, Mario Balotellio
anaonekana hajaacha vituko baada ya kuelezwa atapigwa faini kutokana na kufumwa
akivuta sigara kwenye choo cha treni.
Balotelli alikutwa na mhudumu wa treni akivuta
sigara wakati wakisafiri kwa ajili ya pambano la Seria A dhidi ya Fiorentina
leo Jumapili, pambano hilo lilimalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Hakuna aliyekuwa ameshtukia hali hiyo, hadi mhudumu
huyo kwa kwenye treni alipomuambia Naibu Rais wa AC Milan, Adriano Galliani.
Baada ya kuambiwa, mara moja Galliani alimuagiza M’Baye
Niang ambaye ni swahiba wa Balotelli akamueleze kuwa ameishabainika na atapigwa
faini kwa kitendo hicho.
La Gazzeta dello Sport limesema kitendo hicho
kilionyesha kumuudhi Galliani, lakini Balotelli alirejea katika eneo hilo akiwa
ni mtu mwenye tabasamu kama hakuna kilichotokea.
Kabla ya kutua AC Milan, Balotelli alikuwa Man City
ambako alikuwa akiongoza kwa kuwa mchezaji mwenye vituko zaidi kuliko wote
wanaoshiriki Ligi Kuu England.
0 COMMENTS:
Post a Comment