April 7, 2013






Uongozi wa Yanga utakutana na kujadili na mwisho kupata jibu ni aina gani ya uwanja inataka kati ya ramani nne ilizopewa na wajenzi wa Kichina.


Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zimeeleza, suala hilo limekuwa ni siri kubwa na baada ya siku saba, jibu litarudishwa kwa Wachina hao hao.


“Tutakutana na kujadili kuhusiana na suala hilo, unajua Yanga ina wataalamu wengi ambao wangependa kuamua mambo yao kwa ushirikiano na kukubaliana.

“Kila mtu atakuwa na nafasi ya kutoa maoni yake kwa kuwa pamoja na ramani zile tatu, lazima suala la gharama litaangaliwa na tutachagua.
“Mwisho tutawasiliana na hao Wachina na kuwaambia tumechagua ramani ipi na nini kinafuatia baada ya hapo,” kilisema chanzo.

Siku chache zilizopita, Kampuni ya Wachina ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG) iliwapa Yanga ramani ya viwanja vitatu, cha gharama zaidi kikiwa kinagharibu dola 50,000 (zaidi ya Sh bilioni 81) ili wachague wanachokihitaji.

 Ramani nyingine thamani yake ilikuwa ni milioni 40,000 yenye uwezo wa kuchukua watu 40,000 na ya mwisho ni thamani yake ni dola milioni 30,000 yenye uwezo wa kuchukua watu 30,000.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic