Timu ya Azam FC inatarajiwa kutua nchini
kesho (Mei 6, mwaka huu) saa 7 mchana kwa ndege ya Emirates kutoka Morocco ikipitia
Dubai ambako ilibadili ndege.
Azam FC ilikuwa nchini Morocco
kucheza mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya AS FAR Rabat ya huko
na kulala kwa mabao 2-1.
Kutokana na kupoteza mchezo huo,
Azam FC imeondolewa katika michuano hiyo kwa kuwa katika mechi ya awali dhidi
ya Waarabu hao wa Morocco matokeo yalikuwa suluhu.
Hata hivyo, Azam FC watalazimika
kujilaumu wenyewe kwa kuwa walifanikiwa kupata penalti lakini ikapotezwa na
John Bocco.
Kama wangefanikiwa kutoa sare ya
aina yoyote ya mabao, Azam FC wangefuzu na kuendelea kuwa wawakilishi pekee wa
Tanzania na Afrika Mashariki katika michuano ya kimataifa.
0 COMMENTS:
Post a Comment