Samatta akiwa mpira na kipa wa Orlando.. |
Pamoja
na kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Orlando Pirates ikiwa kwenye uwanja
wake wa nyumba, TP Mazembe imetolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa
Afrika.
Mazembe
anayochezea Mtanzania, Mbwana Ally Samatta imetolewa kwa kuwa ilitakiwa
kushinda mabao 2-0 ili kusonga mbele baada ya kuwa imepoteza kwa mabao 3-1
katika mechi ya kwanza jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
Mazembe
walipoteza mkwaju wa penalty, bado nahodha wa Orlando Pirates, Lucky Lekgwath
akalambwa kadi nyekundu katika dakika ya 28.
Mazembe
walifunga bao lao katika dakika ya 73 kupitia kwa Kasusula lakini wenyeji hao
walipoteza mikwaju miwili ya penati yote ikipanguliwa na kipa wa Pirates, Senzo
Meyiwa.
Mkwaju
wa kwanza wa penalti uliotolewa na mwamuzi kutoka Shelisheli ulipigwa na Eric
Bokanga kipa huyo akaokoa, mkwaju wa pili akapiga nyota wa Mazembe, Tresor
Mputu nao ukapanguliwa na kipa huyo.
Pamoja
na hivyo Mazembe bado walishindwa kuzitumia nafasi walizozipata kupata bao hilo
ambalo lingewavusha.
Mitandao
ya Afrika Kusini iliripoti kwamba kuna mwandishi mmoja amekamatwa na kukataliwa
kurekodi mechi hiyo na alikuwa anashikilia hadi baada ya mchezo huo.
0 COMMENTS:
Post a Comment