May 17, 2013



Saa 24 tu baada ya kutwaa ubingwa wa Europa League, wachezaji wa Chelsea akiwemo Frank Lampard, Juan Mata na Oscar wamezawadiwa tuzo nyingine.


Hafla ya tuzo hizo ilifanyika jana usiku na wachezaji hao wakazawadiwa kutokana na kazi yao katika klabu hiyo ambayo imetwaa makombe mawili makubwa barani Ulaya katika miaka miwili.



Katika sherehe ya tuzo hizo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, Mata alilamba tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Chelsea ikiwa ni kwa mara ya pili mfululizo.


Kiungo Mbrazil, Oscar alishinda tuzo ya vao bora la msimu na kinda, Nathan Ake aliteuliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka anayechipukia.
Frank Lampard naye alikabidhiwa tuzo ya heshima ya kuweka rekodi ya kufunga mabao mengi na kuvunja rekodi ya Bobby Tambling.

Chelsea ilifanikiwa kushinda mabao 2-1 dhidi ya Benfica mjini Amsterdam na kubeba kombe hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic