May 16, 2013



 
Saanya akiwa kazini katika mechi kati ya Coastal dhidi ya Yanga, msimu uliopita mjini Tanga.
Mwamuzi Martin Saanya atakayechezesha pambano la watani Simba na mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga, Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ni askari magereza.

Salehjembe limebaini kazi ya Saanya ambaye ni askari wa jeshi hilo mkoani Morogoro na aliyebadilishwa Israel Mujuni Nkongo ni mwalimu.

Saanya ndiyo mwamuzi wa mchezo huo na tayari Simba imeandika barua TFF kupinga mwamuzi huyo kuingizwa katika nafasi ya Nkongo, tena ghafla.


Mwamuzi huyo ilikuwa kazi kumpata, kila alipopigiwa simu hakupokea lakini kachero wa Salehjembe alifanikiwa kumnasa mjini Morogoro, naye akazungumzia mchezo huo kwa kifupi tu.

“Najua ni mchezo ambao unatazwa na watu wengi sana, nitakachofanya ni kufuata haki tu na si vingine,” alisema Saanya akikataa kuzungumza zaidi.

Baadhi ya rafiki zake wa karibu hasa wale waamuzi pia, walimtambulisha Saanya kama mwamuzi anayefuata sheria sana, asiyekubali kuyumbishwa.

Hivyo wachezaji wa Yanga na Simba wanapaswa kuwa makini kwani anaweza asisite kumwaka kadi kama njugu kama wachezaji hao hawatacheza soka na kuleta ‘mambo mengine’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic