May 19, 2013




Kocha Mkuu wa Yanga, Ernies Brandts amesema kikosi chake kilicheza vizuri na anawapongeza wachezaji kwa uwezo mkubwa waliouonyesha.

Lakini amekiri kwamba Chuji ndiye alistahili kuwa mchezaji bora wa mchezo kama walivyotangaza Supersport.

“Timu yangu inafanya kila kitu kama timu, tunashinda na kupoteza pamoja. 

“Lakini kitaalamu kuna mambo mengi sana, kuwa mchezaji bora we mechi ni kitu cha kawaida na wala kisiwakatishe tamaa wengine.


“Chuji alistahili kuwa mchezaji bora wa mchezo huo kwa kuwa alifanya kaiz kubwa.

“Kwanza nasema bado kuna mambo ya kufanya Yanga, ninaamini msimu ujao tunaweza kufanya vizuri zaidi,” alisema.

Salehjembe ilikuwa ya kwanza kumtangaza Chuji kuwa mchezaji bora wa mechi ya watani, Yanga na Simba, juzi kwenye Uwanja wa taifa, Dar.

Chuji alicheza kama kiungo mkabaji na alichezesha timu huku akiongoza kwa kukaba na kuwapa ahueni kubwa walinzi wa kati, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic