May 16, 2013



 
 Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga wanatarajia kutua jijini Dar es Salaam kimyakimya wakitokea Pemba walikoweka kambi ya siku kadhaa kujiandaa na mechi dhidi ya watani wao Simba.

Yanga inashuka dimbani kucheza na Simba keshokutwa Jumamosi katika mechi ya kufunga pazia la Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuwa kali nay a kuvutia.

Taarifa ambazo Salehjembe imezipata, Yanga itatua kesho asubuhi  au mchana na kuweka kambi katika hoteli moja maarufu jijini Dar.

Kinachowarudisha Yanga siku moja kabla ya mechi ni kuhakikisha wanafanya mazoezi kwenye uwanja wenye nyasi halisi kama zle watakazozitumia kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi.


Yanga imekuwa ikifanya mazoezi kwenye nyasi bandia mjini Pemba, hivyo inaonekana kwao ni vema kufanya angalau kwa siku moja kwenye nyasi halisi.

Hata hivyo, uongozi wa Yanga umefanya safari hiyo siri kubwa na hautaki ijulikane wanarudi lini.

Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema hivi: “Bado tuko huku Pemba, suala la kuja lini wanajua zaidi ni kamati ya utendaji.
“Lakini hapa Pemba ratiba ya mazoezi asubuhi.

“Kama ni nyasi bandia hata Azam wamekuwa wakifanya katika nyasi bandia na kucheza katika nyasi za kawaida.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic