May 12, 2013




Dakika chache baada ya kuukosa Ubingwa wa FA kwa kuchapwa na Wigan, Kocha Mkuu Man City, Roberto Mancini amesema uzushi mtupu umetawala kuhusiana na nafasi yake kutaka kuchukuliwa na Kocha wa Malaga, Manuel Pellegrini.

Lakini Mancini ameushambulia uongozi wa Man City kwamba haukuonyesha juhudi zozote kwamba suala hilo ni uzushi kwa kufungua mdomo na kulizungumzia.

“Naweza kusema huo ni upuuzi,” alisema Mancini alipozungumza na kituo cha runinga cha ITV cha Uingerreza baada ya mechi dhidi ya Wigan.
 

“Bado siwezi kujua ni kweli au la, lakini katika soka kila kitu kinaweza kutokea. Lakini klabu imekaa kimya, haikusema lolote kuhusiana na hilo kuonyesha kuzuia kuendelea kwa tetesi hizo, si kitu kizuri.”

“Bado nna miaka minne katika mkataba wangu, kama itakuwa kweli kuhusiana na Pellegrini ni kweli, basi mimi ntakuwa mpuuzi.”
Hivi karibuni ilielezwa uongozi wa Man City kupitia mmoja wa viongozi  alikutana na wakala wa Pellegrini na kujadili naye suala la kutua kuifundisha timu hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic