May 21, 2013

Kocha Mkuu mpya wa Uganda, Sredojevich Milutin ‘Micho’ amesema atafanya makubwa akiwa na kikosi hicho maarufu kama The Cranes.
 Micho raia wa Serbia, ambaye hivi karibuni ametimuliwa kuinoa Rwanda, Amavubi amepewa nafasi ya kuinoa Uganda na atakuwa akisaidiwa na kocha mwingine wa zamani wa Yanga, Sam Timbe.


Micho amesema anaamini Uganda ni sawa na nyumbani kwa kuwa alifanya kazi kwa kipindi kirefu wakati akiinoa SC Villa, hivyo aliamini siku moja angerudi.

Akizungumza na Salehjembe kutoka Kampala, Micho alisema anatamani kuanza kazi hata leo.

“Hapa nimerudi nyumbani, natamani nianze kazi hata leo. Lakini kitu kikubwa ambacho ninaamini nitafanya vizuri na Uganda.

“Najua soka la Uganda, nawajua wachezaji pia najua Waganda wanataka ushindi na wako tayari kuisaidia timu yao ya taifa.

“Hivyo kila kitu kitakwenda vizuri kama wote kwa pamoja tukitaka wafanye hivyo,” alisema Micho.

“Awali nilitaka kuja Tanzania kuangalia mechi ya Yanga na Simba, lakini nilishindwa kutokana na kuwa katika mazungumzo ya mwisho na Fufa.
“Bado naendelea kuwashukuru watu wa Rwanda, hasa walioshirikiana nami, lakini nguvu zote nazielekeza katika kazi mpya.”

Micho aliwahi kuinoa Yanga wakati ikishiriki Ligi Ndogo mwaka 2008, Timbe pia alikuwa kocha wa Yanga mwaka juzi na kuipa ubingwa wa Kombe la Kagame.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic