| Nikiwa na Cafu wa Brazil, jamaa nilimhoji hata bila ya kupangiwa na hakuwa na noma.. |
Maisha ni safari ya aina yake, najaribu kukumbuka siku kadhaa zilizopita, sasa zinaonekana ni miaka tena.
| Saleh Ally na Marcelo Lippi baada ya mahojiano, alikuwa amekasirika baada ya waandishi wa Italia nao kulazimisha afanye mahojiano nao bila ya kufuata utaratibu... |
Afrika Kusini ilifanya vizuri zaidi ya Ulaya, lakini bahati kwangu kama mwandishi wa habari.
| Baada ya kumaliza kushiriki katika upangaji wa ratiba za Kombe la Dunia mwaka 2010 jijini Cape Town. |
Katika kuchagua, nilimchagua kocha wa mabingwa kutoka Italia, Marcelo Lippi. Alinipa ushirikiano mkubwa na mahojiano yangu yalikuwa bomba sana.
| Nikipiga danadana nje ya Cape Town Stadium kabla haujakamilika.. |
Hakika nilijifunza mengi, najua ni vigumu kupata bahati kama hizo, lakini nilijifunza kumbe hata bahati hutafutwa, haziji ukiwa umelala nyumbani.
NAKUMBUKA ZAMANI!







0 COMMENTS:
Post a Comment