May 21, 2013




Na Mwandishi Wetu
SHABIKI mmoja wa Simba, ameshindwa kujizuia na kuangua kilio mbele ya Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts.

Mfanyakazi huyo aliangua kilio wakati Brandts alipoamua kwenda kupata mlo wake katika hoteli moja maarufu eneo la Masaki jijini Dar es Salaam.

Baada ya kumuona Brandts, shabiki huyo haraka alimkimbilia na kumueleza kwamba anasikia uchungu sana kuhusiana na Yanga kuifunga Simba kwa mabao 2-0 siku moja iliyopita.


Shabiki huyo alimueleza Brandts kwamba yeye ni Simba damu, lakini amejitokeza kumpongeza Mholanzi huyo kutokana na kazi nzuri aliyoifanya.

“Kweli amenishangaza,” alisema Brandts baada ya shabiki huyo kuangusha chozi. “Lakini ameonyesha kiasi gani ni shabiki wa dhati wa Simba na anayekubali kazi waliyoifanya Yanga.

“Soka ndiyo iko hivyo, chochote kinaweza kutokea. Lakini kama kutakuwa na watu wanakubali kazi za wenzao kama yule shabiki, basi hata maana ya soka itaonekana.”

Brandts aliondoka siku hiyo na kurejea kwao Uholanzi ambako atakuwa katika mapumziko hadi mwanzoni mwa mwezi ujao atakaporejea na kuanza maandalizi ya michuano ya kimataiga na msimu mpya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic