June 27, 2013




Bao lililofungwa kwa kichwa na Paulinho katika dakika ya 86, limeipeleka Brazil hadi fainali ya michuano ya Kombe la Mabara.

Brazil imefanikiwa kutinga fainali baada ya kuifunga Uruguay kwa jumla ya mabao 2-1.

Brazil walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 41 kupitia Fred baada ya kazi nzuri ya Neymar lakini Uruguay wakasawazisha katika dakika ya 48 baada ya mabeki wake kufanya makosa na mara moja Cavani akafunga.

Mechi hiyo ilikuwa ni ya vuta nikuvute na Uruguay ndiyo walianza kupata nafasi ya kufunga baada ya mwamuzi kuwapa mkwaju wa penalty baada ya David Luiz kufanya madhambi ndani ya 18.

Lakini mkwaju wa mkongwe Diego Forlan ukaolewa na kila Julio na kufanya ugumu wa mechi uendelee hadi mwisho Brazil walipofanikiwa kuibuka na ushindi.








0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic