August 9, 2013



Lucy Mgina na Martha Mboma
KIPA wa Taifa Stars, Juma Kaseja amesema ameshindwa kusaini mkataba wa kujiunga na FC Lupopo ya DR Congo kwa kuwa wahusika wa klabu hiyo walimkabidhi ukiwa umeandikwa kwa Lugha ya Kifaransa.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Kaseja alisema alipelekewa mkataba ambao alitakiwa kuusaini, baada ya kuuangalia akiwa na watu wake wanaomsimamia, wakakuta umeandikwa kwa Lugha ya Kifaransa ambayo wao hawaifahamu.

“Mkataba ulikuja kwa Kifaransa, tukawataka wakautafsiri kwa lugha ambayo sisi tutaielewa kisha waulete tena ili uonyeshe yale tuliyoyataka kama yamo.

“Kuna watu wananisimamia kila kitu katika hili na ilikuwa ngumu kusaini kwa kuwa hatujui kilichoandikwa kwa sababu kuna mambo inabidi tuyaelewe kabla sijasaini,” alisema Kaseja ambaye ni kipa wa zamani wa Simba.  

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic