August 9, 2013



Richard Bukos na Lucy Mgina
KOCHA wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime amesema sababu kubwa ya kumsajili mshambuliaji Musa Hassan Mgosi (pichani) ni kuimarisha safu yake ya ushambuliaji lakini atamtumia zaidi kama mwalimu kwa wenzake kwa kuwa yeye ni mzoefu.

Maxime amesema kuwa ana imani Mgosi atatumia uzoefu wake kuwa kioo kwa wenzake hasa chipukizi ili kuipa faida klabu hiyo. Nimeamua kuwachukua wachezaji kadhaa wakongwe akiwemo Mgosi ambaye hata mimi nimecheza naye ili kuimarisha kikosi changu na kumtumia kama kocha wa uwanjani,” alisema Maxime.

Naye Kocha Msaidizi wa Mtibwa, Zuberi Katwila alisema: “Mgosi tumemsajili kwa kuwa tunajua atatusaidia msimu ujao, tumempa mkataba wa mwaka mmoja.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic