August 9, 2013



Na Wilbert Molandi
KUONDOKA kwa kiungo mshambuliaji wa Simba, Mwinyi Kazimoto (pichani kushoto) kumeikosesha Klabu ya Simba mamilioni kutokana na kuelezwa kuwa, mchezaji huyo alikuwa akitakiwa na Klabu ya FC Porto ya Ureno.

Kazimoto amesaini mkataba wa kuichezea Al-Markhiya Sports Club ya Qatar, wiki hii kwa dau la dola 50,000 (Sh milioni 80), ikiwa ni mkataba wa mwaka mmoja.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pope amesema kiungo huyo amechukua maamuzi ya haraka lakini kama angeendelea kubaki Simba kwa muda, angepata dili hilo la kusajiliwa na klabu hiyo ya Ureno ambao anadai walitoa ahadi ya kutoa donge nono zaidi.

“Kazimoto amechukua maamuzi ya haraka ya kwenda kucheza soka la kulipwa Qatar, alitakiwa kusubiri kutokana na ofa tulizokuwa tunazipata kutoka Ulaya.

“FC Porto ilionyesha nia ya kumsajili hivi karibuni, lakini akatoroka na kwenda huko Qatar kwenye majaribio, timu hiyo iliahidi kutoa dau kubwa la usajili na mshahara zaidi ya huo atakaoenda kuupata Qatar,” alisema Hans Pope.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic