Mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe
ameonyesha kuchanganyikiwa na kushindwa kuzungumza.
Tambwe raia wa Burundi alilazimika
kutimua mbio pamoja na wachezaji wengine wa Simba pia wale wa Kagera Sugar,
sekunde tu baada ya mwamuzi kupuliza filimbi ya mwisho ya mchezo wa leo kati
yao.
Mashabiki wa Simba walianza kufanya
vurugu wakipinga penalty iliyotolewa na mwamuzi huyo na Kagera wakasawazisha
bao.
Wakati wachezaji wanakimbilia vyumbani,
Tambwe alikataa kuzungumza huku akionekana ni mwenye hofu.
Katika mechi hiyo, Tambwe alizidi
kujichimbia kileleni kwa kufunga bao la tisa.
Tambwe amefunga bao la tisa, siku moja
tu baada ya Hamisi Kiiza wa Yanga, raia wa Uganda kufikisha mabao nane.
0 COMMENTS:
Post a Comment