October 31, 2013

MALINZI AKIWA NA MMOJA WA WATU WAKE WA NGUVU

Rais mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema kati ya mambo atakayoanza nayo ni soka la wanawake.
Malinzi amesema katika mipango ya muda mfupi atakayoanza nayo ni soka la wanawake.


“Tutahakikisha timu ya wanawake chini ya miaka 20 inasonga mbele na baada ya hapo, tutaendelea na maandalizi mengine.
“Hakuna namna, lazima tuwaunga mkono kwa wakati huu kwa kuwa wao ndiyo wako vitani na wanaliwakilisha taifa.

“Suala hilo nitaanza nalo katika mipango ya muda mfupi, lakini baada ya hapo itakuwa ni mipango ya muda mrefu ambayo inajumuisha mambo mengi kama kusaka vipaji, vifaa, soka mashuleni na mambo mengine mengi,” alisema Malinzi.

Timu ya taifa ya Wanawake chini ya miaka 20, Tanzania iliitungua Msumbiji kwa mabao 10-0 katika mechi ya kwanza kuwania kucheza Kombe la Dunia iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar na sasa ni maandalizi kwa ajili ya marudiano mjini Maputo.

Malinzi amechukua nafasi hiyo iliyokuwa inashikiliwa na Leodeger Tenga baada ya kumshinda Athumani Nyamlani.


Tayari Tenga amesema atamkabidhi Malizi ofisi rasmi keshokutwa saa tano asubuhi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic