Miss World 2003, Rosanna Davison ameingia
mkataba kutangaza katika televisheni ya LFC TV inayomilikiwa na klabu ya
Liverpool.
Mwandada huyo mwenye miaka 29, binti wa
mwanamuziki Chris de Burgh wa Ireland pia ni mwanamitindo na mtangazaji maarufu
nchini Ireland.
Ameingia mkataba huo na Liverpool na
utakuwa wa kwanza kwake nje ya nchi yake na sasa analazimika kuhamia jijini Liverpool,
England.
Tayari mwandada huyo ameishatengeneza
vipindi viwili vya dakika 30 kila kimoja na vitaanza kurushwa hivi karibuni.
0 COMMENTS:
Post a Comment