October 8, 2013







Baada ya kupoteza mechi mbili nyumbani, Mgambo Shooting iko ugenini kesho (Oktoba 9 mwaka huu) kuikabili Azam katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.


Mgambo Shooting yenye pointi tano, ikiwa nafasi ya pili kutoka mwisho imeshinda mechi moja tu dhidi ya Ashanti United huku ikipoteza mbili nyumbani dhidi ya JKT Ruvu na Tanzania Prisons. 

Kocha Mohamed Kampira ana kibarua cha kuhakikisha anapata pointi mbele ya Azam.

Mechi nyingine za ligi hiyo ni Rhino Rangers itacheza na Mbeya City kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati JKT Ruvu watakuwa wageni wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Manungu uliopo Turiani mkoani Morogoro.

Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha utakuwa shuhuda wa mechi kati ya wenyeji Oljoro JKT na Ruvu Shooting ya Pwani inayofundishwa na Charles Boniface Mkwasa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic