Mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe
amesema atacheza katika mechi ya leo dhidi ya Kagera Sugar kama makocha
Abdallah Kibadeni na Jamhuri Kihwelo wataona anastahili kufanya hivyo.
Simba inashuka dimbani leo katika mechi ngumu ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar.
Tambwe ambaye anaongoza kwa kufunga
mabao na sasa akiwa sawa na Hamis Kiiza wa Yanga, amesema amepania kucheza
mechi hiyo lakini ni uamuzi wa walimu hao.
“Walimu ndiyo wataamua, maana nimekuwa
nikisumbuliwa na maumivu na siku moja ya juzi nilikaa nje bila ya kufanya
mazoezi.
“Ndiyo maana nasema walimu wataamua
kuhusiana na hilo, mimi niko tayari kucheza kwa kuwa nataka kushirikiana na
wenzangu kuisaidia timu yetu,” alisema Tambwe.
Tokea alipofunga bao la nane wiki tatu
zilizopita, Tambwe hajafunga tena na hivi karibuni Kiiza amemfikia na kuwa sawa
naye kwa mabao nane kila mmoja na ndiyo wanaoongoza listi ya wafungaji bora.
Kiukweli huwa siridhiki na unavyoripoti taarifa zako. Uko-bias sana, huwezi na kwa hili huwezi kudumu wana huwezi kuacha legacy kwenye Tasnia ya Habari; kwa hali hii huwezi compite even within East Africa . Try be professional...
ReplyDelete