Uongozi wa Azam umekubaliana kwa pamoja
kusitisha mipango yote ya usajili mpaka kocha wao mpya, Joseph Omog, raia wa
Cameroon, atakapofika.
Taarifa ambazo Championi Jumatano limezipata
kutoka ndani ya Azam FC, zimesema uongozi wa timu hiyo umeona usitishe zoezi la
kusajili au kuwaacha nyota wa timu hiyo,
mpaka kocha wao huyo atakapowasili na kuiona timu.
Bosi mmoja (jina tunalo), amesema tayari
timu hiyo ilikuwa na majina ya nyota waliotakiwa kusajiliwa katika kikosi hicho
pamoja na wale wanaoachwa. Kufuatia mapendekezo aliyoyafanya awali aliyekuwa
kocha wa timu hiyo, Muingereza, Stewart Hall, kazi hiyo imesitishwa mpaka kocha
mpya atakapoleta tathmini yake.
“Asikwambie mtu kwamba tunasajili
mchezaji yeyote kwa sasa, Azam kama unavyoona tupo kimya tukisubiri kwanza
kocha wetu mpya afike ili atupe kile anachokiona katika timu, aongezewe kipi na
kipi kiondolewe,” alisema bosi huyo na kuongeza:
“Uongozi wetu hautaki kumsajilia kocha
wachezaji, mpaka sasa tulikuwa na mapendekezo mbalimbali aliyoyafanya Stewart
kabla ya kutangaza kuondoka, lakini hakuna kitakachofanyika katika hilo,”
kilisema chanzo hicho.
SOURCE: CHAMPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment