CHACHA ALIPOKUWA YANGA |
Beki wa zamani wa Yanga, Chacha Marwa,
Jumamosi ya wiki iliyopita alizichapa na mshambuliaji wa zamani wa Simba, Ally
Ahmed Shiboli, kwenye mechi ya kuwania Kombe la Ng’ombe iliyopigwa katika
Uwanja wa Sinai, Vingunguti jijini Dar.
Chanzo cha karibu na wachezaji hao
kilisema Chacha alikuwa akiichezea Faru Jeuri na Shiboli akiwa na Soweto.
SHIBOLI ALIPOKUWA SIMBA |
Chacha wakati akigombea mpira alipigwa kichwa na Shiboli hadi akamchana mdomo, hali iliyomkasirisha beki huyo wa kati na kuamua kwenda kumrushia ngumi Shiboli na ndipo vurugu zilipoanza.
Alisema hata hivyo, Shiboli naye alikuja
juu na vita ikaanza lakini mashabiki na viongozi wa timu hizo waliwahi na
kuwaamua.
Hata hivyo, baada ya kuwaamua, mashabiki
walimvamia mwamuzi wa mchezo huo ambaye ni mchezaji wa zamani wa Yanga na
Simba, Ephraim Makoye, kwa madai kuwa anapendelea.
Baada ya vurugu hizo, Makoye alitoka
nduki na filimbi yake mkononi hali iliyosababisha mchezo huo kuvunjika.
“Mechi haikuisha kutokana na vurugu iliyoanzia
kwa wachezaji Chacha na Shiboli ambao walipigana uwanjani, hivyo mpira ukasimama
kwa ajili ya kuwaamua lakini tukashangaa na refa naye wanampiga wakati hakuwa
na kosa lolote.
Ikabidi akimbie na mpira
ukawa umeishia hapohapo dakika ya 77 huku kina Shiboli wakiongoza kwa bao 1-0,”
kilisema chanzo.
0 COMMENTS:
Post a Comment