Muda mchache ujao kipa Yaw Berko raia wa
Ghana atasaini mkataba wa miezi sita kuichezea Simba katika mzunguko wa pili.
Kipa huyo mzoefu ametua nchini asubuhi
hii badala ya jana jioni kama ilivyokuwa imelezwa hapo awali.
Hata hivyo, Berko hakutaka kuzungumza
masuala mengi zaidi badala yake amesisitiza aachiwe hadi hapo atakapokutana na
uongozi wa Simba.
“Nitazungumza zaidi hapo baadaye baada
ya kuzungumza na viongozi na kujua ni I hasa tunakwenda kufanya na mwisho wake
ni nini,” alisema.
Simba imekuwa ikihaha kumsaka kipa
mzoefu baada ya uongozi kufikiak uamuzi wa kuachana na Mganda Abel Dhaira
ambaye kiwango chake kimeporomoka.
0 COMMENTS:
Post a Comment