Katibu Mkuu wa zamani wa timu ya Simba, Hassan Othman ‘Hassanoo’ leo ameshinda kesi ya wizi
wa shaba ya zaidi ya shilingi milioni 300.
Kesi hiyo iliyokuwa ikimkabili kwenye mahakama
ya Kisutu jijini Dar es salaam, ilihudhuriwa na watu wengi kwa kuwa walijua leo ni siku ya hukumu.
Katika kesi hiyo mshitakiwa wa pili alikuwa ni
baba mkwe wa Hassanoo aitwae Dokta Najim Kisega na mshitakiwa wa tatu alikuwa
Wambura Mahenya Kisiroti.
Baada ya hakimu, Sundi Fimbo kuwaachia huru wote watatu
maafande wa Jeshi la Magereza waliendelea kumng'ang'ania Hassanoo kwa ajili ya
kesi ya meno ya tembo na mwisho wakamrudisha gerezani.
PICHA NA RICHARD BUKOS WA CHAMPIONI/GPL
PICHA NA RICHARD BUKOS WA CHAMPIONI/GPL
0 COMMENTS:
Post a Comment