Na Mwandishi Wetu, Nairobi
Rais mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), Jamal Malinzi ameitwa ili kukaa na kujadiliana na shirikisho la hapa KFF
ili kuboresha nguvu ya maendeleo katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Rais wa Shirikisho la Soka Kenya (KFF),
Sam Nyamweya amesema anaamini Malinzi ni kati ya watakaochangia kasi ya
maendeleo ya soka katika ukanda huu.
Akizungumza nyumbani kwake jijini hapa, Nyamweya alisema
Malinzi ni kati ya watu anaoamini watanga vizuri kwa kuwa ni mchapakazi.
“Tayari nimeandaa utaratibu ikiwezekana
nikutane na Malinzi, tujadili masuala kadhaa kwa ajili ya maendeleo pamoja kama
nchi za Afrika Mashariki na baadaye nitafanya hivyo kwa Uganda, Rwanda na
Burundi.
“Inawezekana kabisa kufanya kitu vizuri
mkiwa pamoja, kila upande utafanya juhudi kuendelea sehemu husika na baada ya
hapo tunachangia kama ukanda wetu.
“Itakuwa kazi ngumu sana kuendelea na
kushindana na Kaskazini na Magharibi mwa Afrika kama tutaendelea kutengana na
kila mmoja anafanya mambo yake tu,” alisema Nyamweya.
“Hata kama kuna tatizo na tunaona Caf
wanatusumbua au kuna kitu kinatukandamiza, inaweza kufikia wakati tukapiga
kelele pamoja na kupinga.”
Alisema kuhusiana na mwaliko wa Malinzi,
atawasiliana naye na kuangalia ligi atakuwa na nafasi naye pia lini ana nafasi,
halafu atalifanyia kazi.
0 COMMENTS:
Post a Comment