Hatimaye Halmashauri ya Jiji la Mwanza imetuma dola 118,000 (Sh milioni
190) kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kwa ajili ya kuweka nyasi
bandia na ujenzi wa majukwaa kwenye Uwanja wa Nyamagana.
Fedha hizo zimetumwa Fifa kupitia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuchangia
mradi huo ambao gharama zake zinafikia dola 618,000 (Sh 990m), tayari Fifa ilishatoa
dola 500,000 (Sh 800m).
Meya wa Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula amesema fedha hizo zilitolewa mwanzoni mwa mwezi huu.
Fifa ilitaka Mwanza ichangie kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kuanza uwekaji wa nyasi hizo bandia katika uwanja huo mkongwe.
Wakati fulani serikali ilitaka kujenga hoteli kubwa katika eneo la uwanja huo lakini ikapata upinzani mkubwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment