Kocha Msaidizi wa Kagera Sugar, Mrage
Kabange amesema walimshauri aliyekuwa kipa wao, Andrew Ntalla, asiende Simba
kwa kuwa kiwango chake kilikuwa bado lakini akakaidi na sasa hawana mpango naye
hata kama atahitaji kurejea klabuni hapo.
Kabange
amesema awali kipa huyo waliyemtoa timu ya Magereza iliyokuwa ikishiriki Ligi
Daraja la Tatu Sumbawanga walimshauri na kumtaka asubiri kwanza kwa kuwa
kiwango chake kilikuwa hakijafikia kuichezea Simba lakini akabisha.
“Sisi tulimshauri kama wazazi wake
lakini hakutuelewa basi tukamuacha tu, si unajua walimwengu wanasema mtoto
akililia wembe mpe nasi tukamuacha,” alisema Kabange.
Aliongeza hawawezi kumrudisha tena
Kagera kwa kuwa wao tayari wana makipa watatu ambao ni Hannington Kalyesabula,
Agatoni Antony na mwingine ambaye wamempandisha kutoka U 20.
0 COMMENTS:
Post a Comment