Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),
Jamal Malinzi, ametamka kuwa kuna mabadiliko yatafanyika katika ngazi ya
uongozi katika taasisi hiyo, lakini akakanusha taarifa kwamba wapo mbioni kumpa ajira aliyekuwa Kocha
wa Azam, Stewart Hall, na kusisitza ajira za wengine ikiwemo ya Mkurugenzi wa
Ufundi, Sunday Kayuni, bado ipo salama.
Malinzi amesema hakuna mazungumzo yoyote kati ya uongozi wake na Stewart kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Kayuni.
“Hatuko katika mazungumzo yoyote na Stewart
juu ya kuchukua nafasi ya Ukurugenzi wa Ufundi, nafasi hiyo ina mtu anayeendelea
na majukumu yake mpaka hapo tutakapofanya maamuzi mengine.
“Bado kuna watendaji ambao wana mikataba
yao, nafikiri tunatakiwa kusubiri, wakati utakapofika tutangaza nafasi zilizo
wazi ili kuweza kuruhusu wengine kuomba,” alisema Kayuni.
0 COMMENTS:
Post a Comment