Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen amemtangaza Aggrey Morris wa
Azam FC kuwa ndiye nahodha mpya wa kikosi hicho.
Taifa Stars hivi sasa ipo kambini ikijiandaa na mechi ya kirafiki dhidi
ya Kenya, Harambee Stars, Jumanne ijayo. Hivyo, Morris atakuwa amechukua nafasi
ya Juma Kaseja aliyekuwa nahodha.
Kim alisema cheo hicho ni cha Taifa Stars na siyo cha kikosi cha
Kilimanjaro Stars, hivyo badala yake hivi sasa anatafuta mchezaji mwingine
atakayempa unahodha kwenye Michuano ya Chalenji itakayofanyika Nairobi, Kenya.
“Cheo hicho atakitumikia akiwa Stars, hivi sasa natafuta nahodha
mwingine wa Kilimanjaro maana Aggrey yeye yupo Zanzibar Heroes,” alisema Kim.
0 COMMENTS:
Post a Comment