Imani ya kocha wa Al Markhiya kwa kiungo
Mtanzania, Mwinyi Kazimoto imezidi kuwa juu.
Kwani Kazimoto ndiye aliyekabidhiwa
jukumu la kuichezesha timu hiyo ya daraja la pili nchini Qatar.
Kocha huyo ameamuamini Kazimoto katika
mechi zote tisa na amekuwa kiungo tegemeo sasa.
Mtanzania huyo alianza kuonyesha dalili
za kuaminiwa na kocha huyo tokea alipotua akitokea Simba.
Akizungumza kutoka Qatar, Kazimoto
alisema ligi ni ngumu na ina changamoto nyingi.
“Ni ligi ngumu sana, lakini katika soka
ushindani upo. Lakini ninapambana na kwa kuwa kocha kaniamini basi najituma
zaidi,” alisema.
Ligi zote nchini humo zimesimama kupisha kikosi chao cha timu ya taifa ambacho kimeingia kambini.
0 COMMENTS:
Post a Comment