Wachezaji kadhaa wa Arsenal waliamua kupoza maumivu kwa kwenda
kushuhudia mechi ya fainali ya Kombe la Barclays ATP kwenye Uwanja wa Wimbledon
jijini London kati ya Novak Djokovic dhidi ya Rafael Nadal.
Djokovic alichukua ubingwa huo kwa kumchapa Nadal bila ya huruma
kwa seti mbili za moja kwa moja za 6-3, 6-4.
WILSHERE (KUSHOTO) |
ARTETA NA KITU CHAKE |
Wakati wakali wakichuana, Jack Wilshere na Mikel Arteta wa Arsenal
walikuwa kati ya mashabiki waliojitokeza.
Wawili hao walicheza katika mechi ya Ligi Kuu England dhidi ya Man
United ambayo Arsenal ililala kwa bao 1-0, pamoja na kucheza vizuri zaidi.
Hivyo ilionekana wawili hao waliamua kujipoza na kushuhudia mechi
hiyo ya wachezaji wakali zaidi duniani iliyoisha kwa Djokovic kuendelea
kuonyesha kweli yeye ni namba 1 sahihi.
0 COMMENTS:
Post a Comment