Kocha mkongwe nchini Abdallah ‘King’ Kibadeni
amekubali kutua na kuifundisha Ashanti United ambayo iko katika wakati mgumu.
Ashanti iko katika wakati mgumu katika
msimamo wa Ligi Kuu Bara na imemaliza mzunguko wa kwanza ikiwa katika nafasi ya
12 kati ya timu 14.
Habari za uhakika kutoka ndani ya
Ashanti zimeeleza, tayari mazungumzo kati ya Kibadeni na kocha huyo
yamefanyika, naye ameridhia kutua huko.
“Tayari mazungumzo yamefanyika, naweza
kusema ni asilimia 90 tuko katika makubaliano na Kibadeni na amekubali kuja
kuifundisha timu yetu. Amesema lile agizo la Rage kumrudisha yeye amelikataa na
hatabaki Simba,” kilieleza chanzo.
“Kwa kuwa ametuhakikishia, basi
tumeanza kuandaa kila anachotaka na tunasubiri tu amalizane na Simba kuchukua
haki yake ili aanze kazi hapa Ashanti.”
Alipotafutwa Kibadeni, jana mchana,
alikiri kufanya mazungumzo na Ashanti lakini akasisitiza suala hilo litabaki
kuwa siri.
“Kweli siwezi kubaki Simba, huo ni
ukweli. Lakini kuhusiana na Ashanti na mambo mengine yote ya Simba
nitayazungumza Jumamosi.
“Nimeitisha mkutano na waandishi wa
habari, nimewaomba waje kwangu Madale, saa nne kamili asubuhi. Nitaeleza kila
kitu kuhusiana na Simba na hata Ashanti, hivyo leo siwezi kuzungumza zaidi,”
alisema Kibadeni.
Kibadeni na msaidizi wake, Jamhuri
Kihwelo ‘Julio’ walifukuzwa kazi na kamati ya utendaji lakini mwenyekiti
aliyesimamishwa, Ismail Aden Rage akawarudisha na kujirudisha madarakani
akisema kamati hiyo haikufuata katiba.
0 COMMENTS:
Post a Comment