Mshambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe
amesema anatumia muda wake wa mapumziko kuwa bize kusimamia ujenzi wa nyumba
yake nchini Burundi katika Mji wa Makamba.
Tambwe alisajiliwa Simba msimu huu
akitokea katika kikosi cha Vital O’ ya Burundi. Tayari amefunga mabao 10 kwenye
Ligi Kuu Bara.
Akizungumza na gazeti hili kutoka
Burundi, straika huyo alisema: “Nipo bize kusimamia ujenzi wa nyumba yangu kwa
sababu ndiyo muda muafaka wa kufanya hivyo kabla sijarejea Tanzania.
“Nyumba hiyo ninayojenga ipo maeneo ya
Makamba, lakini hata Bujumbura nina uwanja pia, wasifikiri Simba ndiyo
imenijengea ila nina mipango yangu ya muda mrefu ambayo nilikuwa nikiiweka
sawa.”
0 COMMENTS:
Post a Comment