Siku chache baada ya kuibuka ghafla kwenye mazoezi ya mabingwa wa
Kenya, Gor Mahia, Kocha Mkuu wa timu ya taifa, Harambee Stars, Adel Amrouche
safari hii amekwenda bila taarifa kwenye shule moja jijini Nairobi.
Amrouche raia wa Ubelgiji aliibukia katika shule hiyo bila ya
mwaliko na kuwashangaza walimu na wanafunzi waliokuwa wakicheza soka.
AKISHUHUDIA WATOTO HAO.. |
AKIKARIBISHWA NA KOCHA WA TIMU HIYO YA SHULE |
Baada ya hapo alishuhudia mazoezi na baada ya hapo akaungana nao
na kuwapa ushauri.
Kocha huyo aliwashauri mambo kadhaa huku akiwapa moyo kwamba kama
wakijituma siku moja watakuwa wachezaji wakubwa na maarufu duniani.
AKITOA NASAHA.. |
Kocha wa timu hiyo alishukuru sana huku akimuambia Amrouche: “Hii
ni mara ya kwanza kwa kocha mkubwa kama wewe kuja katika mazoezi yetu, ni kitu
kikubwa kwetu na hawa watoto.
“Hata viongozi wetu wamekuwa wakipita tu hapa lakini hakuna hata
mmoja ambaye amewahi kuja kutuona.”
SIKU CHACHE ALIPOIBUKA KWENYE MAZOEZI YA GOR MAHIA
AKIMUAGA KOCHA WA GOR MAHIA, BOBBY WILLIAMSON |
AKIWA NA MOSES ODHIAMBO |
AKIWA NA LAVTSA |
0 COMMENTS:
Post a Comment